Friday, November 6, 2009

MAPENDEKEZO/USHAURI YA MAREKEBISHO YA SHERIA

MSWADA WA SHERIA YA HAKI YA MTOTO WA 2009(UPANDE WA WAPINZANI)
1)Haki ya kutoa maoni
2)Tafsiri ya mtoto
3)Chombo cha kusimamia sheria n.k

MAPENDEKEZO/USHAURI YA MAREKEBISHO YA SHERIA

MSWADA WA SHERIA YA HAKI YA MTOTO WA 2009(WABUNGE WA KAMATI YA MAENDELEO YA JAMII
1)Tafsiri ya mtoto.
2)Sehem ya kutunzia watoto wadogo iongezwe.
3)Mlezi kumpatia mtoto haki yake ya msingi/mirasi.
4)Serikali itenge sehemu maalumu ya michezo (kucheza watoto).
5)Wazazi,walezi,watoe ushirikiano kwa mtoto aliyepotea.
6)Mahakama za watoto zitengwe mbali na mahakama za watuwazima ili kutoa huoga kwa watoto kujielezea

Wednesday, October 28, 2009

MH.NAGU AZUNGUMZA NA WAZAZI

DAR ES SALAAM,

WAZAZI nchini wanatakiwa kuwazoeza watoto kujenga tabia ya kujisomea vitabu vya ziada na vile vya kiada ili kujenga taifa lenye viongozi wazuri hapo baadae.

Wito huo umetolewa ivi karibuni na Waziri wa Viwanda na Masoko Mary Nagu alipokuwa anafungua tamasha la 18 la Taifa la maonyesho ya vitabu kwenye Ukumbi wa Ubungo Plaza Wilayani Kinondoni.

Waziri Nagu amesema kuwa kasi ya Watanzania katika usomaji wa vitabu bado hauridhishi kutokana na wengi wao kutumia muda mwingi kwenye shughuli nyingine pamoja na starehe hivyo kukosa muda wa kusoma vitabu au kuwahimiza watoto kufanya hivyo.

Hata hivyo Waziri Nagu amekiri kuwa Serikali haijaiwezesha vizuri tasnia ya vitabu nchini ingawa inafanya jitihada za kuandaa mazingira mazuri kwenye tasnia hiyo ili ifanye vizuri.

Tamasha hilo lenye kauli mbiu SOMA VITABU UJIENDELEZE, UJIKOMBOE litaendelea kwa muda wa wiki moja na linajumuisha wadau mbalimbali wa vitabu nchini na nchi nyingine za Afrika Mashariki pamoja na Rwanda.

Thursday, October 22, 2009

MTOTO AFA KWA KUKEKETWA

Na Jamillah wa MAJIRA
POLISI Mkoani Manyara wanamshikilia Bw.Danieli Shauri(37)kwa kosa la kumkeketa binti yake,Debora Daniel (4) na kumsababishia kifo.
Mtoto huyo alikeketwa oktoba 11,mwaka huu na kuendelea kuvuja damu sehemu za siri hadi oktoba 18 alipofariki dunia.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa manyara,Parmena Sumary alisema kuwa tukio hilo limetokea siku hiyo saa 10.00 jioni katika kijiji cha Imbilili Wilayani Babati.
Kamanda Sumary alisema kabla ya kifo chake,mtoto huyo alikuwa akiishi na mtuhumiwa baada ya mama yake mzazi,Bi.Catherine Daniel(29)kupata kichaa na kumtelekeza akiwa mdogo.
Kutokana na hali hiyo mtoto alikosa afya na kupata homa za marakwa mara kwasababu ya kukosa maziwa ya mama,hali iliyosababisha wazazi wa mtuhumiwa kushauri akeketwe ili kuondokana na matatizo hayo.
Kamanda alisema kuwa mtuhumiwa alitekeleza ushauri potofu wa wazazi wake,lakini alishangazwa na hali ya mtoto huyo kuendelea kuwa mbaya hadi alipofariki dunia kwa kupoteza damu nyingi.
Baada ya kifo hichokutokea,mtuhumiwa alitaka kuuzika mwili wa mtoto huyo bila ya watu kujua lakini wasamaria walitoa taarifa kwa mtendaji wa kijiji hicho,Patizimu Joseph ambaye alifika nyumbani kwa mtuhumiwa na kukuta maandalizi ya mazishi na kuwaamuru kusimamisha shughuli hiyo hadi hatua za kisheria zitakapofuatwa
Baada ya amri hiyo mwili huo ulichukuliwa hadi hospitali ya wilwya ya Babati kwa uchunguzi zaidi na ndipo iligundulika kuwa marehem alipatwa na mauti hayo baada ya kukeketwa na kuvuja damu nyingi.
Kwa mujibu wa kamanda huyo,ngariba aliyehusika kumkeketa mtoto huyo,Mama Mangiza,alitoroka baada ya hali ya mtoto na polisi wanaendelea kumsaka kujibu shtaka hilo.

Friday, October 9, 2009

DAR ES SALAAM

WAZIRI wa Maendeleo ya jamii,jinsia na watoto,Bibi Margareth Sitta,amesema kupitia sheria mpya ya haki ya mtoto,walezi watakaobainika kuwanyanyasa watoto watalipishwa faini kati ya shilingi 500,000 hadi milioni mbili.

Waziri Sitta,amesema sheria hiyo ya mwaka 2009,ndiyo itakayokomesha unyanyasaji wa watoto unaofanywa hivi sasa na baadhi ya walezi nchini ambao umekithiri katika jamii.

waziri Sitta,ametoa kauli hiyo ivi karibuni wakati wa mjadala kuhusu mswada wa sheria hiyo uliohusisha wadau husika kabla ya kuwasilishwa bungeni

Amesema,awali kulikuwa hakuna sheria madhubuti inayolinda haki ya mtoto nchini,lakini kupitia sheria hiyo ana imani kuwa haki hizo sasa zitapatikana ipasavyo na kukomesha unyanyasaji huo

Waziri Sitta,amesema sheria hiyo imeainisha haki zote za mtoto hivyo vituo na walezi wakiwemo mama wakambo watakaokiuka haki hizo watachukuliwa hatua za kisheria.

Friday, September 18, 2009

DAR ES SALAAM,

Walimu nchini watakiwa kujenga tabia ya kufanya tafiti mbalimbali za kisayansi, kiuchumi, na kiutamaduni kwa vile kwa kufanya hivyo kutawasaidia kuboresha maisha yao pamoja na jamii inayowazunguka.

Wito huo umetolewa na leo na Mkurugenzi Mkuu wa wa kampuni yakuchapisha vitabu na magazeti ya Bussiness Printers Limited Bwana Rashidi Mbuguni alipokua akifungua semina ya siku moja inayolenga kuwawezesha walimu wa masomo ya hesabu na biashara kwa ngazi ya Sekondari kufundisha kwa vitendo.


Bwana Mbuguni amesema kuwa umefika wakati ambao walimu nchini wanatakiwa watumie vitendo zaidi ya maelezo ikiwa ni pamoja na kuandaa vitabu vya masomo wao wenyewe badala ya kutegemea vitabu kutoka nje ya nchi kwa vile haviendani sana na mazingira ya kitanzania.

Kwa upande wao walimu wa somo la hesabu Mkoani Dar es salaam,wamesema kuwa ni muda mrefu wamekuwa wakioomba Wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi stadi kuwaruhusu kuandaa vitabu vyao kwa vile vitabu vingi wanavyotumia vina makosa mengi.

Semina hiyo ya siku moja imedhaminiwa na kampuni ya Bussiness Printers Limited na imeanza kwa mkoa wa Dar es salaam na baadae kuendelea mikoa yote nchini ambapo kampuni hiyo imetoa udhamini wa uchapishji wa vitabu kwa masomo ya hesabu na biashara.
DAR ES SALAAM,

Bwana Madaraka Nyerere ambaye ni mtoto wa rais wa zamani Tanzania Hayati Mwl. Julius Nyerere pamoja na Jaffar Amini ambaye ni mtoto wa raisi wa zamani wa Uganda Iddi Amin kwa pamoja wanatarajia kupanda mlima Kilimanjaro kwa ajili ya kuchangisha fedha za hisani kuwasaidia watoto yatima wanaolelewa na asasi isiyo ya kiserikali ya Community Alive iliyoko mjini Musoma.

Akizungumza na waandishi wa habari leo kwenye Ukumbi wa Idara ya habari Maelezo Bwana Madaraka Nyerere amesema hatua hiyo pia inalenga kumuenzi baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere ambapo kwa pamoja wanatarajia kuanza kupanda mlima huo Octoba 29 hadi Novemba 6 mwaka huu.

Bwana Madaraka amewaomba wananchi mbalimbali kuchangia asasi hiyo ili kufanikisha lengo lake la kuwasaidia watoto hao ambao wameachwa na wazazi wao kutokana na ugonjwa wa Ukimwi kupitia namba ya akaunti 064-6000246 kwenye benki ya Barclays tawi la Musoma kupitia jina la Community Alive.

Hii ni mara ya pili kwa Bwana Madaraka kuchangisha fedha za hisani ambapo mwaka jana alifanikiwa kuchagisha kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 22 zilizowezesha ujenzi wa mabweni ya shule ya Sekondari ya wasichana ya Mtemi Edward Wanzagi iliyopo mkoani Mara.

Hayati Mwalimu Nyerere na Iddi Amini walikuwa na tofauti kubwa za kisiasa kitu kilichopelekea kuvunjika kwa iliyokuwa jumuiya ya Afrika Mashariki mwaka 1977 na chanzo cha vita vya Kagera mwaka 1979.

JAMII YAHIMIZWA KUSAIDIA YATIMA ELIMU

TAASISI na kampuni zimehimizwa kusaidia watoto yatimana wanaoishi katika mazingira magumu,ili waweze kutimiza ndoto zao maishani.
Mwiti huo ulitolewa jana na Dar es salaam na Mkurugenzi wa kituo cha kulelea watoto wanaoishi katika mazingira magumu na yatima cha Mkakuya Ophans na Vulnerable Children Center,Cecilia Nasoro,wakati akipokea msaada wa futari kutoka kampuni ya simu Tanzania(TTCL).
Kampuni hiyo ilitoa msaada wa vitu mbalimbali vyenye thamani ya zaidi ya sh.milioni tano kwa vituo vinne vya kulelea watoto.Mbali na Mkakuya vingine ni Msongora Ophans Trust Fund, vilichoko Mbagala,Mama Teresa na Nuruhud Madrasat vya Mburahati,Dar es salaam
Wakati akipokea msaada huo,Nasoro alisema misaada ya watoto hao isiishie kutoa vyakula na mambo mengine,isipokuwa sasa kampuni,taasisi na jamii zijizatiti kutoa udhamini wa elimu na ajira salama kwa watoto hao.

Friday, September 11, 2009

MWALIMU WA SHULE YA MSINGI ASHIKILIWA KWA KUVUJISHA MTIHANI

MWALIMU Mkuu katika shule Msingi Kiziko wilayani Mkuranga,Silvester Undole(48)ameunganishwa na walimu wengine wawili wanaoshikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuvujisha mtihani wa taifa wa darasa la saba uliomalizika juzi.
Mkamanda wa polisi mkoa wa Pwani,Absalom Mwakyomo,alisema Undole ambaye alikuwa msimamizi wa mtihani katika shule ya msingi Lupondo,alikamatwa jana baada yakirudisha karatasi pungufu za mitihani hiyo.
"Mwalimu huyu anadaiwa kutoa karatasi za maswali kwa walimu wawili tunaowashikilia wa Lupondo ambao waligawa majibu kwa wanafunzi hao".
Alisema upelelezi wa awali ulibaaini kuwa Undole alikabidhiwa karatasi hizo 32 lakini alirudisha 31 kabla ya kukamatwa kwake.
Alisema mtuhumiwa huyo na watuhumiwa wenzake wawili ambao ni Hamis Katundu (51)na Musa Mayotela(49)walitarajiwa kufikishwa katika mahakama ya Wilaya ya Mkuranga kwa ajili ya kujibu tuhuma zinazowakabili
Mkuu wa Mkoa wa Pwani,Hajati Amina Said alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa uchunguzi unaendelea

Saturday, September 5, 2009

WANAFUNZI KUJIPELEKA WENYEWE POLISI

MKUU wa mkoa wa Pwani,Bi.Amina saidi,amewataka wanafunzi wa kike ambao watashindwa kuwataja wanaume wanaosababisha ujauzito,kujipeleka wenyewe polisi.
Bibi Amina,ametoa kauli hiyo wakati wa ziara yake katika shule ya wasichana ya Tumbi inayomilikiwa na Shirika la Elimu Kibaha,mkoani Pwani
Bibi Amina amesema kuwa baadhi ya wanafunzi wa kike hawapo tayari kuwataja wanaume wanaowasababishia mimba hizo,haliambayo licha ya kuwakatisha masomo,laikini pia inasababisha Serikali kushindwa kuwachukulia hatua watuhumiwa hao.

Friday, September 4, 2009

WATOTO YATIMA WASAIDIWE

WAMILIKI wa shule binafsi na mashirika ya kidini nchini wameshauriwa kutenga nasafi za upendeleo kwa watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu ili kuwanusuru katika majanga mbalimbali.
Akizungumza jana mjini Dodoma,Mkurugenzi wa Rhema Academy Pre and Primary School,Neema Majule alisema kuwa jukumu la kuwalea watoto hao ni la kila Mtanzania,hivyo inatakiwa kujitolea kwa hali na mali.
"Licha ya shule zetu kuwa za kibiashara,mwito wangu kwa wamiliki ni kuwa tutenge hata nafasi kidogo ili tuweze kuwasaidia na hawa watoto"alisema.
Alisema shule hiyo ina wanafunzi yatima na wanaoishi katika mazingira magumu zaidi ya 20 ambao wanasoma bure wakigharamiwa ada,chakula,mavazi,na usafiri

Thursday, September 3, 2009

WALIMU WATAKIWA KUBADILIKA

WALIMU Mkoani Shinyanga wametakiwa kuipenda na kuiheshimu kazi yao ikiwa ni pamoja na kubadilika katika utendaji wa kazi zao ili kuondokana na aibu ambayo huikumba mkoa huo kwa kufanya vibaya katika mitihani ya kitaifa kwa shule zao.
Wito huo ulitolewa hivi karibuni katika eneo la Mwanhuzi Wilaya ya Meatu na Kaimi Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu,Bi.Georgia Machumu wakati akifungua mafunzo ya walimu wa shule za msingi nchini.
Bi.Machumu alisema kuwa wakati umefika kwa kila mwalimu shuleni kuhakikisha anabadilika na kutambuwa wajibu wake na dhamana kubwa katika taifa hili kwa kuondoa adui mjinga.

Saturday, August 29, 2009

KORTINI KWA MAUWAJI IDODI

MWANAFUNZI wa kidato cha tatu shule ya sekondari Idodi,mkoani Iringa Erick Mnyali(16),anayedaiwa kusababisha moto bweni la wasichana la shule hiyo na kuua wanafunzi 12,amefikishwa katika mahakama ya Mkoa wa Iringa kwa makosa 12 ya kuua bila kukusudia.
Mtuhumiwa huyo alipandishwa katika mahakama hiyo majira ya saa 8.30 alasiri jana na kesi yake inasomwa kuwa mauaji namba 29 ya mwaka 2009.
Mbele ya hakimu wa mahakama hiyo,Geofrey Mhini,Mwendesha mashitaka Mratibu wa Polisi,Mwenda alidai kuwa mtuhumiwa alitenda makosa hayo Agost 23,mwaka huu.

Friday, August 28, 2009

JELA MIAKA 30 KWA KUNAJISI

MKAZI wa Buguruni Kisiwani Deogratias Joseph Lyimo(27) amehukumiwa miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya kubaka.

Kabla hakimu Janeth kinyage wa mahakama ya wilaya ya Ilala kutoa hukumu hiyo,Mwendesha mashitaka wa polisi,Inspekta Mussa Gumbo,aliiomba Mahakama kutoa adhabu kali kwa mshitakiwa ili kukomesha vitendo kama hivyo katika jamii.

Hakimu Kinyange amesema kuwa kutokana na maelezo yaliyotolewa mahakamani hapo na pande zote mbili,mahakama imemuhukumu mshitakiwa kutumikia kifungo miaka hiyo ili iwe fundisho kwa wengine.

Mh.MAHIZA AWAWAKIA WALIMU

NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya ufundi Bi.Mwantumu Mahiza amesema ole wake mwalimu atakayebainika kufungia vitabu katika kabati lake badala ya kuwagawia wanafunzi wajisomee na kujifunza mambo mbalimbali.
Alitoa onyo hilo kwa walimu wa sekondari na msingi hivi karibuni,baada ya kutembelea shule mbalimbali za msingi na sekondarikatika Wilaya ya Sumbawanga Mkoani Rukwa na kugundua kuwa baadhi ya walimu wanalalamikia upungufu mkubwa wa vitabu...Bi.Mahiza alisema ni jambo la ajabu hata majarida mbalimbali yanayotolewa na taasasa mbalimbaliyanayoelezea kuhusu UKIMWI yamefungiwa bila kuwagawia wanafunzi wanaopaswa kuwa na uelewa kuhusu ugonjwa huo.
"Jamani vitabu si mali ya mwalimu bali ni mali ya mwanafunzi hivyo ni lazima vitabu vyote vitoke maofisini na kuwafikia walengwa ambao ni wanafunzi na nasema kuwa agizo hili si kwa Sumbawanga pekee bali ni kwa nchi nzima"alisema Bi.Mahiza

Tuesday, August 18, 2009

Bi.Ngoye ANENA NA WAZAZI

MBUNGE wa viti maalumu(ccm)kutoka mkoa wa Mbeya Bi.Hilda Ngoye ametaka wanafunzi wanaopeana mimba wakiwa shuleni wote wafukuzwe kwa pamoja ili kujenga nidhamu kwa vijana wengine.
Hayo yamezungumzwa wakati akihutubia wazazi na wanafunzi katika kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya shule ya sekondari ya wazazi META ya jijini Mbeya jumamosi Agost 15 mwaka huu.
Bi.Ngoye amesema kuwa kukithiri kwa vitendo vya ujauzito katika shule za msingi na sekondari husababishwa na jinsia zote hivyo inapobainika aliyempa mwanafunzi mimba ni mwanafunzi mwenzie naye anapaswa kuwajibika
"Wanafunzi wa kike wanaopewa mimba na wale wanaosababisha mimba wote wanatakiwa kutimuliwa.........hii itakuwa njia mbadala ya kukomesha wimbi la mimba baina ya wanafunzi kwa wanafunzi".alisema Bi.Ngoye

Thursday, August 13, 2009

MATATANI KWA KUTOMASA NYETI ZA CHEKECHEA

MSHITAKIWA Omary Amiry miaka 40 mkazi wa Mbezi kwa Msuguli amefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni kujibu mashitaka ya kumshikashika mtoto wa kike wa miaka 6 sehemu zake za siri.

Mbele ya Hakimu Hilda Lyatuu imedaiwa na mwendesha mashitaka Inspeta wa polisi Benedict Nyagabona kuwa,Julai 21 mwaka huu,mshitakiwa kwa makusudi alimshikashika mtoto huyo.

Mshitakiwa alikana mashitaka hayo na kesi hiyo itatajwa tena Agosti 26 mwaka huu.

Tuesday, August 11, 2009

WARATIBU ELIMU KATA WATAKIWA KUZUNGUMZA NA WAZAZI

WARATIBU Elimu kata nchini wametakiwa kuwaelimisha wazazi kuhusu uhusiano mzuri kati ya walimu,wasimamizi wa shule na wazazi ili mwalimu awe na mazingira mazuri ya kufanya kazi.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Karatu,Bw.Mathew Sedoyeka wakati akifunga semina ya waratibu elimu kata wa wilaya za Karatu,Ngorongoro na manispa ya Arusha iliyofanyika wilayani humo,

ASKOFU MTOKAMBALI SISITIZA MALEZI BORA

ASKOFU Mkuu wa kanisa la Tanzania Assemblis of God(TAG),Dkt.Barnabas Mtokambali amewasisitiza wazazi kuhusu malezi bora kwa watoto wao ili kujenga jamii yenye maadili mema.

Kiongozi huyo wa dini alisema ni jukumu la kila mzazi kuhakikisha kuwa mtoto wake anapata malezi bora ili kuweza kuwajengea msingi mzuri wa maisha ya badae.

Askofu Mtokambali alisema hayo juzi wakati akihubiri katika kanisa la City Center lililoko jijini Tanga na kuwataka waumuni wa kanisa hilo kudumisha upendo miongoni mwao na waumini wa dini nyingine nchini ili kulinda amani na utulivu iliyopo hapa nchini.

Aliongeza kuwa ni vema waumini wa kanisa hilo wakaendelea kuimarisha upendo na mshikamano uliopo nchini kwa kuwatembelea na kuwasaidia watu walio katika makundi yenye mahitaji maalumu nchini ili nao wazidi kuishi kwa amani mioyoni mwao.

Monday, August 10, 2009

Mwandaaji wa Miss tototo Temeke Jackline Magayane akizungumnza katika shindano la kumsaka Miss tototo mwaka 2009

Fatuma Issa(katikati)akiwa na mshindi wa pili na watatu



Fatuma Issa mshindi wa miss tototo temeke 2009 katika pozi





Miss tototo top 5 katika pozi


Miss tototo wakionyesha shoo ya pamojaMtoto Ashura Omary akipita na vazi la mtoko


Mtoto Fatuma Issa akipita na vazi lake la kutokea



Mtoto Eda Damiani akipita na vazi lake la mtoko




Zaituni Hassani akipita na vazi lake la kutokea


Mtoto Fatuma Issa akiwa katika pozi na vazi la ubunifu
Mtoto Jane Antony akipita na vazi la ubunifu


Mtoto Neema Ally akionyesha vazi lake la ubunifu

Msanii wa kizazi kipya Duly syksi akicheza na watoto katika shindano la kumsaka miss tototo temeke ivi karibuni




Wasanii kutoka wakali Dansa wakionyesha manjonjo wakati wa shindano la miss tototo temeke



Sunday, August 9, 2009

hata sisi jamani tunaweza umiss jamani cheki nilivyo pozi














Friday, August 7, 2009

MSWADA WA SHERIA WA HAKI ZA WATOTO KWA MWAKA 2009

Na:Malela Kassim

Waziri wa Maendeleo ya jamii jinsia na watoto,Bibi Margareth Simwanza Sitta ametoa wito kwa jamii ya Watanzania kuunga mkono hoja inayoitaka Serikali kipitisha sheria inayowahusu watoto wa kike nchini kuendelea na masomo baada ya kujifungua kufuatia kupewa mimba wakiwa bado wanaendelea na masomo.
Akitolea mfano wa nchi za Zambia,Malawi na Zanzibar ambazo zimepitisha na kutumia sheria hiyo Bibi Sitta amesema kuwa nchi hizo zinafanya vizuri kielimu na pia zinawapa watoto wa kike haki ya kupata elimu ambayo ni haki ya kila mtoto ulimwenguni pote.

Kwa upande wake mjumbe wa kushugulikia haki za watoto Nchini Ghana Bibi Agnes Akosua Aidoo ameiomba Serikali ya Tanzania kuhakikisha inatoa bure vyeti vya kuzaliwa kwa kuwa hiyo ni haki ya kwanza ambayo mtoto anatakiwa apewe mara baada ya kuzaliwa.

Mswada huo mpya wa haki za watoto unalenga kuweka Mashirika maalumu kwa ajili ya kuboresha,kuhifadhi na kulinda haki za watoto ili kuhifadhi matakwa ya mikataba ya kimataifa kuhusu haki ya mtoto