Saturday, September 5, 2009

WANAFUNZI KUJIPELEKA WENYEWE POLISI

MKUU wa mkoa wa Pwani,Bi.Amina saidi,amewataka wanafunzi wa kike ambao watashindwa kuwataja wanaume wanaosababisha ujauzito,kujipeleka wenyewe polisi.
Bibi Amina,ametoa kauli hiyo wakati wa ziara yake katika shule ya wasichana ya Tumbi inayomilikiwa na Shirika la Elimu Kibaha,mkoani Pwani
Bibi Amina amesema kuwa baadhi ya wanafunzi wa kike hawapo tayari kuwataja wanaume wanaowasababishia mimba hizo,haliambayo licha ya kuwakatisha masomo,laikini pia inasababisha Serikali kushindwa kuwachukulia hatua watuhumiwa hao.

No comments:

Post a Comment