Friday, August 28, 2009

Mh.MAHIZA AWAWAKIA WALIMU

NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya ufundi Bi.Mwantumu Mahiza amesema ole wake mwalimu atakayebainika kufungia vitabu katika kabati lake badala ya kuwagawia wanafunzi wajisomee na kujifunza mambo mbalimbali.
Alitoa onyo hilo kwa walimu wa sekondari na msingi hivi karibuni,baada ya kutembelea shule mbalimbali za msingi na sekondarikatika Wilaya ya Sumbawanga Mkoani Rukwa na kugundua kuwa baadhi ya walimu wanalalamikia upungufu mkubwa wa vitabu...Bi.Mahiza alisema ni jambo la ajabu hata majarida mbalimbali yanayotolewa na taasasa mbalimbaliyanayoelezea kuhusu UKIMWI yamefungiwa bila kuwagawia wanafunzi wanaopaswa kuwa na uelewa kuhusu ugonjwa huo.
"Jamani vitabu si mali ya mwalimu bali ni mali ya mwanafunzi hivyo ni lazima vitabu vyote vitoke maofisini na kuwafikia walengwa ambao ni wanafunzi na nasema kuwa agizo hili si kwa Sumbawanga pekee bali ni kwa nchi nzima"alisema Bi.Mahiza

No comments:

Post a Comment