Friday, September 4, 2009

WATOTO YATIMA WASAIDIWE

WAMILIKI wa shule binafsi na mashirika ya kidini nchini wameshauriwa kutenga nasafi za upendeleo kwa watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu ili kuwanusuru katika majanga mbalimbali.
Akizungumza jana mjini Dodoma,Mkurugenzi wa Rhema Academy Pre and Primary School,Neema Majule alisema kuwa jukumu la kuwalea watoto hao ni la kila Mtanzania,hivyo inatakiwa kujitolea kwa hali na mali.
"Licha ya shule zetu kuwa za kibiashara,mwito wangu kwa wamiliki ni kuwa tutenge hata nafasi kidogo ili tuweze kuwasaidia na hawa watoto"alisema.
Alisema shule hiyo ina wanafunzi yatima na wanaoishi katika mazingira magumu zaidi ya 20 ambao wanasoma bure wakigharamiwa ada,chakula,mavazi,na usafiri

No comments:

Post a Comment