Friday, September 18, 2009

JAMII YAHIMIZWA KUSAIDIA YATIMA ELIMU

TAASISI na kampuni zimehimizwa kusaidia watoto yatimana wanaoishi katika mazingira magumu,ili waweze kutimiza ndoto zao maishani.
Mwiti huo ulitolewa jana na Dar es salaam na Mkurugenzi wa kituo cha kulelea watoto wanaoishi katika mazingira magumu na yatima cha Mkakuya Ophans na Vulnerable Children Center,Cecilia Nasoro,wakati akipokea msaada wa futari kutoka kampuni ya simu Tanzania(TTCL).
Kampuni hiyo ilitoa msaada wa vitu mbalimbali vyenye thamani ya zaidi ya sh.milioni tano kwa vituo vinne vya kulelea watoto.Mbali na Mkakuya vingine ni Msongora Ophans Trust Fund, vilichoko Mbagala,Mama Teresa na Nuruhud Madrasat vya Mburahati,Dar es salaam
Wakati akipokea msaada huo,Nasoro alisema misaada ya watoto hao isiishie kutoa vyakula na mambo mengine,isipokuwa sasa kampuni,taasisi na jamii zijizatiti kutoa udhamini wa elimu na ajira salama kwa watoto hao.

No comments:

Post a Comment