Saturday, August 29, 2009

KORTINI KWA MAUWAJI IDODI

MWANAFUNZI wa kidato cha tatu shule ya sekondari Idodi,mkoani Iringa Erick Mnyali(16),anayedaiwa kusababisha moto bweni la wasichana la shule hiyo na kuua wanafunzi 12,amefikishwa katika mahakama ya Mkoa wa Iringa kwa makosa 12 ya kuua bila kukusudia.
Mtuhumiwa huyo alipandishwa katika mahakama hiyo majira ya saa 8.30 alasiri jana na kesi yake inasomwa kuwa mauaji namba 29 ya mwaka 2009.
Mbele ya hakimu wa mahakama hiyo,Geofrey Mhini,Mwendesha mashitaka Mratibu wa Polisi,Mwenda alidai kuwa mtuhumiwa alitenda makosa hayo Agost 23,mwaka huu.

No comments:

Post a Comment