Wednesday, October 28, 2009

MH.NAGU AZUNGUMZA NA WAZAZI

DAR ES SALAAM,

WAZAZI nchini wanatakiwa kuwazoeza watoto kujenga tabia ya kujisomea vitabu vya ziada na vile vya kiada ili kujenga taifa lenye viongozi wazuri hapo baadae.

Wito huo umetolewa ivi karibuni na Waziri wa Viwanda na Masoko Mary Nagu alipokuwa anafungua tamasha la 18 la Taifa la maonyesho ya vitabu kwenye Ukumbi wa Ubungo Plaza Wilayani Kinondoni.

Waziri Nagu amesema kuwa kasi ya Watanzania katika usomaji wa vitabu bado hauridhishi kutokana na wengi wao kutumia muda mwingi kwenye shughuli nyingine pamoja na starehe hivyo kukosa muda wa kusoma vitabu au kuwahimiza watoto kufanya hivyo.

Hata hivyo Waziri Nagu amekiri kuwa Serikali haijaiwezesha vizuri tasnia ya vitabu nchini ingawa inafanya jitihada za kuandaa mazingira mazuri kwenye tasnia hiyo ili ifanye vizuri.

Tamasha hilo lenye kauli mbiu SOMA VITABU UJIENDELEZE, UJIKOMBOE litaendelea kwa muda wa wiki moja na linajumuisha wadau mbalimbali wa vitabu nchini na nchi nyingine za Afrika Mashariki pamoja na Rwanda.

No comments:

Post a Comment