Friday, August 28, 2009

JELA MIAKA 30 KWA KUNAJISI

MKAZI wa Buguruni Kisiwani Deogratias Joseph Lyimo(27) amehukumiwa miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya kubaka.

Kabla hakimu Janeth kinyage wa mahakama ya wilaya ya Ilala kutoa hukumu hiyo,Mwendesha mashitaka wa polisi,Inspekta Mussa Gumbo,aliiomba Mahakama kutoa adhabu kali kwa mshitakiwa ili kukomesha vitendo kama hivyo katika jamii.

Hakimu Kinyange amesema kuwa kutokana na maelezo yaliyotolewa mahakamani hapo na pande zote mbili,mahakama imemuhukumu mshitakiwa kutumikia kifungo miaka hiyo ili iwe fundisho kwa wengine.

No comments:

Post a Comment