Thursday, August 13, 2009

MATATANI KWA KUTOMASA NYETI ZA CHEKECHEA

MSHITAKIWA Omary Amiry miaka 40 mkazi wa Mbezi kwa Msuguli amefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni kujibu mashitaka ya kumshikashika mtoto wa kike wa miaka 6 sehemu zake za siri.

Mbele ya Hakimu Hilda Lyatuu imedaiwa na mwendesha mashitaka Inspeta wa polisi Benedict Nyagabona kuwa,Julai 21 mwaka huu,mshitakiwa kwa makusudi alimshikashika mtoto huyo.

Mshitakiwa alikana mashitaka hayo na kesi hiyo itatajwa tena Agosti 26 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment