Friday, October 9, 2009

DAR ES SALAAM

WAZIRI wa Maendeleo ya jamii,jinsia na watoto,Bibi Margareth Sitta,amesema kupitia sheria mpya ya haki ya mtoto,walezi watakaobainika kuwanyanyasa watoto watalipishwa faini kati ya shilingi 500,000 hadi milioni mbili.

Waziri Sitta,amesema sheria hiyo ya mwaka 2009,ndiyo itakayokomesha unyanyasaji wa watoto unaofanywa hivi sasa na baadhi ya walezi nchini ambao umekithiri katika jamii.

waziri Sitta,ametoa kauli hiyo ivi karibuni wakati wa mjadala kuhusu mswada wa sheria hiyo uliohusisha wadau husika kabla ya kuwasilishwa bungeni

Amesema,awali kulikuwa hakuna sheria madhubuti inayolinda haki ya mtoto nchini,lakini kupitia sheria hiyo ana imani kuwa haki hizo sasa zitapatikana ipasavyo na kukomesha unyanyasaji huo

Waziri Sitta,amesema sheria hiyo imeainisha haki zote za mtoto hivyo vituo na walezi wakiwemo mama wakambo watakaokiuka haki hizo watachukuliwa hatua za kisheria.

No comments:

Post a Comment